Islamic Vault

Quran

89

Al-Fajr

سورة الفجر

The Dawn30 Verse Mekkanisch

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ وَالْفَجْرِ

Naapa kwa alfajiri,

2

وَلَيَالٍ عَشْرٍ

Na kwa masiku kumi,

3

وَالشَّفْعِ وَالْوَتْرِ

Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,

4

وَاللَّيْلِ إِذَا يَسْرِ

Na kwa usiku unapo pita,

5

هَلْ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِذِي حِجْرٍ

Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?

6

أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ

Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?

7

إِرَمَ ذَاتِ الْعِمَادِ

Wa Iram, wenye majumba marefu?

8

الَّتِي لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِي الْبِلَادِ

Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?

9

وَثَمُودَ الَّذِينَ جَابُوا الصَّخْرَ بِالْوَادِ

Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?

10

وَفِرْعَوْنَ ذِي الْأَوْتَادِ

Na Firauni mwenye vigingi?

11

الَّذِينَ طَغَوْا فِي الْبِلَادِ

Ambao walifanya jeuri katika nchi?

12

فَأَكْثَرُوا فِيهَا الْفَسَادَ

Wakakithirisha humo ufisadi?

13

فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ

Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.

14

إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ

Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.

15

فَأَمَّا الْإِنْسَانُ إِذَا مَا ابْتَلَاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَنِ

Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!

16

وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلَاهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ

Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!

17

كَلَّا ۖ بَلْ لَا تُكْرِمُونَ الْيَتِيمَ

Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,

18

وَلَا تَحَاضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ

Wala hamhimizani kulisha masikini;

19

وَتَأْكُلُونَ التُّرَاثَ أَكْلًا لَمًّا

Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,

20

وَتُحِبُّونَ الْمَالَ حُبًّا جَمًّا

Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.

21

كَلَّا إِذَا دُكَّتِ الْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا

Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,

22

وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا

Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,

23

وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الْإِنْسَانُ وَأَنَّىٰ لَهُ الذِّكْرَىٰ

Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?

24

يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي

Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!

25

فَيَوْمَئِذٍ لَا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ

Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.

26

وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌ

Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.

27

يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ

Ewe nafsi iliyo tua!

28

ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَرْضِيَّةً

Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.

29

فَادْخُلِي فِي عِبَادِي

Basi ingia miongoni mwa waja wangu,

30

وَادْخُلِي جَنَّتِي

Na ingia katika Pepo yangu.

Islamic Vault

Quran Explorer

Eine umfassende Online-Ressource zum Lesen und Studieren des Heiligen Korans mit mehreren Übersetzungen, Transliterationen und Audiorezitationen von renommierten Rezitatoren.

Dies ist das Buch, an dem kein Zweifel ist, eine Rechtleitung für die Gottesfürchtigen.

Koran 2:2

Funktionen

  • Audiorezitationen
  • Mehrere Übersetzungen
  • Transliterationen
  • 114 Suren
  • 6.236 Verse

© 2026 Islamic Vault. Alle Rechte vorbehalten.

Mit Ehrfurcht und Sorgfalt für das Buch Allahs erstellt

Entwickelt von Medita Development

Haftungsausschluss: Obwohl wir uns um Genauigkeit bemühen, überprüfen Sie bitte wichtige religiöse Informationen bei authentischen islamischen Gelehrten und Quellen. Diese Plattform dient Bildungszwecken.