Islamic Vault

Quran

88

Al-Ghaashiya

سورة الغاشية

The Overwhelming26 Verse Mekkanisch

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ

Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?

2

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ خَاشِعَةٌ

Siku hiyo nyuso zitainama,

3

عَامِلَةٌ نَاصِبَةٌ

Zikifanya kazi, nazo taabani.

4

تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةً

Ziingie katika Moto unao waka -

5

تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ آنِيَةٍ

Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.

6

لَيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِنْ ضَرِيعٍ

Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.

7

لَا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِي مِنْ جُوعٍ

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

8

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَاعِمَةٌ

Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.

9

لِسَعْيِهَا رَاضِيَةٌ

Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,

10

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ

Katika Bustani ya juu.

11

لَا تَسْمَعُ فِيهَا لَاغِيَةً

Hawatasikia humo upuuzi.

12

فِيهَا عَيْنٌ جَارِيَةٌ

Humo imo chemchem inayo miminika.

13

فِيهَا سُرُرٌ مَرْفُوعَةٌ

Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,

14

وَأَكْوَابٌ مَوْضُوعَةٌ

Na bilauri zilizo pangwa,

15

وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌ

Na matakia safu safu,

16

وَزَرَابِيُّ مَبْثُوثَةٌ

Na mazulia yaliyo tandikwa.

17

أَفَلَا يَنْظُرُونَ إِلَى الْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ

Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?

18

وَإِلَى السَّمَاءِ كَيْفَ رُفِعَتْ

Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?

19

وَإِلَى الْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ

Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?

20

وَإِلَى الْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ

Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?

21

فَذَكِّرْ إِنَّمَا أَنْتَ مُذَكِّرٌ

Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.

22

لَسْتَ عَلَيْهِمْ بِمُصَيْطِرٍ

Wewe si mwenye kuwatawalia.

23

إِلَّا مَنْ تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ

Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,

24

فَيُعَذِّبُهُ اللَّهُ الْعَذَابَ الْأَكْبَرَ

Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!

25

إِنَّ إِلَيْنَا إِيَابَهُمْ

Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.

26

ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُمْ

Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!

Islamic Vault

Quran Explorer

Eine umfassende Online-Ressource zum Lesen und Studieren des Heiligen Korans mit mehreren Übersetzungen, Transliterationen und Audiorezitationen von renommierten Rezitatoren.

Dies ist das Buch, an dem kein Zweifel ist, eine Rechtleitung für die Gottesfürchtigen.

Koran 2:2

Funktionen

  • Audiorezitationen
  • Mehrere Übersetzungen
  • Transliterationen
  • 114 Suren
  • 6.236 Verse

© 2026 Islamic Vault. Alle Rechte vorbehalten.

Mit Ehrfurcht und Sorgfalt für das Buch Allahs erstellt

Entwickelt von Medita Development

Haftungsausschluss: Obwohl wir uns um Genauigkeit bemühen, überprüfen Sie bitte wichtige religiöse Informationen bei authentischen islamischen Gelehrten und Quellen. Diese Plattform dient Bildungszwecken.