Islamic Vault

Quran

90

Al-Balad

سورة البلد

The City20 Verse Mekkanisch

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ لَا أُقْسِمُ بِهَٰذَا الْبَلَدِ

Naapa kwa Mji huu!

2

وَأَنْتَ حِلٌّ بِهَٰذَا الْبَلَدِ

Nawe unaukaa Mji huu.

3

وَوَالِدٍ وَمَا وَلَدَ

Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.

4

لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنْسَانَ فِي كَبَدٍ

Hakika tumemuumba mtu katika taabu.

5

أَيَحْسَبُ أَنْ لَنْ يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌ

Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?

6

يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًا لُبَدًا

Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.

7

أَيَحْسَبُ أَنْ لَمْ يَرَهُ أَحَدٌ

Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?

8

أَلَمْ نَجْعَلْ لَهُ عَيْنَيْنِ

Kwani hatukumpa macho mawili?

9

وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ

Na ulimi, na midomo miwili?

10

وَهَدَيْنَاهُ النَّجْدَيْنِ

Na tukambainishia zote njia mbili?

11

فَلَا اقْتَحَمَ الْعَقَبَةَ

Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

12

وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْعَقَبَةُ

Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?

13

فَكُّ رَقَبَةٍ

Kumkomboa mtumwa;

14

أَوْ إِطْعَامٌ فِي يَوْمٍ ذِي مَسْغَبَةٍ

Au kumlisha siku ya njaa

15

يَتِيمًا ذَا مَقْرَبَةٍ

Yatima aliye jamaa,

16

أَوْ مِسْكِينًا ذَا مَتْرَبَةٍ

Au masikini aliye vumbini.

17

ثُمَّ كَانَ مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا بِالْمَرْحَمَةِ

Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.

18

أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ

Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.

19

وَالَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِنَا هُمْ أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ

Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.

20

عَلَيْهِمْ نَارٌ مُؤْصَدَةٌ

Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.

Islamic Vault

Quran Explorer

Eine umfassende Online-Ressource zum Lesen und Studieren des Heiligen Korans mit mehreren Übersetzungen, Transliterationen und Audiorezitationen von renommierten Rezitatoren.

Dies ist das Buch, an dem kein Zweifel ist, eine Rechtleitung für die Gottesfürchtigen.

Koran 2:2

Funktionen

  • Audiorezitationen
  • Mehrere Übersetzungen
  • Transliterationen
  • 114 Suren
  • 6.236 Verse

© 2026 Islamic Vault. Alle Rechte vorbehalten.

Mit Ehrfurcht und Sorgfalt für das Buch Allahs erstellt

Entwickelt von Medita Development

Haftungsausschluss: Obwohl wir uns um Genauigkeit bemühen, überprüfen Sie bitte wichtige religiöse Informationen bei authentischen islamischen Gelehrten und Quellen. Diese Plattform dient Bildungszwecken.

Surah Al-Balad - Ali Muhsin Al-Barwani Swahili Translation | Islamic Vault | Islamic Vault