İslami Hazine
89

Al-Fajr

سورة الفجر

The Dawn30 ayet Mekki

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ وَالْفَجْرِ

Naapa kwa alfajiri,

2

وَلَيَالٍ عَشْرٍ

Na kwa masiku kumi,

3

وَالشَّفْعِ وَالْوَتْرِ

Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,

4

وَاللَّيْلِ إِذَا يَسْرِ

Na kwa usiku unapo pita,

5

هَلْ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِذِي حِجْرٍ

Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?

6

أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ

Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?

7

إِرَمَ ذَاتِ الْعِمَادِ

Wa Iram, wenye majumba marefu?

8

الَّتِي لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِي الْبِلَادِ

Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?

9

وَثَمُودَ الَّذِينَ جَابُوا الصَّخْرَ بِالْوَادِ

Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?

10

وَفِرْعَوْنَ ذِي الْأَوْتَادِ

Na Firauni mwenye vigingi?

11

الَّذِينَ طَغَوْا فِي الْبِلَادِ

Ambao walifanya jeuri katika nchi?

12

فَأَكْثَرُوا فِيهَا الْفَسَادَ

Wakakithirisha humo ufisadi?

13

فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ

Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.

14

إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ

Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.

15

فَأَمَّا الْإِنْسَانُ إِذَا مَا ابْتَلَاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَنِ

Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!

16

وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلَاهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ

Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!

17

كَلَّا ۖ بَلْ لَا تُكْرِمُونَ الْيَتِيمَ

Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,

18

وَلَا تَحَاضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ

Wala hamhimizani kulisha masikini;

19

وَتَأْكُلُونَ التُّرَاثَ أَكْلًا لَمًّا

Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,

20

وَتُحِبُّونَ الْمَالَ حُبًّا جَمًّا

Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.

21

كَلَّا إِذَا دُكَّتِ الْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا

Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,

22

وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا

Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,

23

وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الْإِنْسَانُ وَأَنَّىٰ لَهُ الذِّكْرَىٰ

Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?

24

يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي

Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!

25

فَيَوْمَئِذٍ لَا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ

Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.

26

وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌ

Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.

27

يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ

Ewe nafsi iliyo tua!

28

ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَرْضِيَّةً

Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.

29

فَادْخُلِي فِي عِبَادِي

Basi ingia miongoni mwa waja wangu,

30

وَادْخُلِي جَنَّتِي

Na ingia katika Pepo yangu.

Islamic Vault

Quran Explorer

Ünlü okuyuculardan çoklu tercümeler, transliterasyonlar ve sesli tilavetlerle Kuran-ı Kerim'i okumak ve incelemek için kapsamlı bir çevrimiçi kaynak.

İşte bu, kendisinde şüphe olmayan kitaptır; Allah'a karşı gelmekten sakınanlar için bir yol göstericidir.

Kuran 2:2

Özellikler

  • Sesli Tilavetler
  • Çoklu Tercümeler
  • Transliterasyonlar
  • 114 Sure
  • 6.236 Ayet

© 2026 İslami Hazine. Tüm hakları saklıdır.

Allah'ın Kitabına saygı ve özenle yapılmıştır

Geliştiren Medita Development

Sorumluluk Reddi: Doğruluk için çaba göstersek de, lütfen önemli dini bilgileri güvenilir İslami alimler ve kaynaklarla doğrulayın. Bu platform eğitim amaçlıdır.