İslami Hazine

Kur'an

90

Al-Balad

سورة البلد

The City20 ayet Mekki

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ لَا أُقْسِمُ بِهَٰذَا الْبَلَدِ

Naapa kwa Mji huu!

2

وَأَنْتَ حِلٌّ بِهَٰذَا الْبَلَدِ

Nawe unaukaa Mji huu.

3

وَوَالِدٍ وَمَا وَلَدَ

Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.

4

لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنْسَانَ فِي كَبَدٍ

Hakika tumemuumba mtu katika taabu.

5

أَيَحْسَبُ أَنْ لَنْ يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌ

Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?

6

يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًا لُبَدًا

Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.

7

أَيَحْسَبُ أَنْ لَمْ يَرَهُ أَحَدٌ

Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?

8

أَلَمْ نَجْعَلْ لَهُ عَيْنَيْنِ

Kwani hatukumpa macho mawili?

9

وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ

Na ulimi, na midomo miwili?

10

وَهَدَيْنَاهُ النَّجْدَيْنِ

Na tukambainishia zote njia mbili?

11

فَلَا اقْتَحَمَ الْعَقَبَةَ

Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

12

وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْعَقَبَةُ

Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?

13

فَكُّ رَقَبَةٍ

Kumkomboa mtumwa;

14

أَوْ إِطْعَامٌ فِي يَوْمٍ ذِي مَسْغَبَةٍ

Au kumlisha siku ya njaa

15

يَتِيمًا ذَا مَقْرَبَةٍ

Yatima aliye jamaa,

16

أَوْ مِسْكِينًا ذَا مَتْرَبَةٍ

Au masikini aliye vumbini.

17

ثُمَّ كَانَ مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا بِالْمَرْحَمَةِ

Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.

18

أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ

Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.

19

وَالَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِنَا هُمْ أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ

Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.

20

عَلَيْهِمْ نَارٌ مُؤْصَدَةٌ

Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.

Islamic Vault

Quran Explorer

Ünlü okuyuculardan çoklu tercümeler, transliterasyonlar ve sesli tilavetlerle Kuran-ı Kerim'i okumak ve incelemek için kapsamlı bir çevrimiçi kaynak.

İşte bu, kendisinde şüphe olmayan kitaptır; Allah'a karşı gelmekten sakınanlar için bir yol göstericidir.

Kuran 2:2

Özellikler

  • Sesli Tilavetler
  • Çoklu Tercümeler
  • Transliterasyonlar
  • 114 Sure
  • 6.236 Ayet

© 2026 İslami Hazine. Tüm hakları saklıdır.

Allah'ın Kitabına saygı ve özenle yapılmıştır

Geliştiren Medita Development

Sorumluluk Reddi: Doğruluk için çaba göstersek de, lütfen önemli dini bilgileri güvenilir İslami alimler ve kaynaklarla doğrulayın. Bu platform eğitim amaçlıdır.