İslami Hazine
88

Al-Ghaashiya

سورة الغاشية

The Overwhelming26 ayet Mekki

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ

Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?

2

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ خَاشِعَةٌ

Siku hiyo nyuso zitainama,

3

عَامِلَةٌ نَاصِبَةٌ

Zikifanya kazi, nazo taabani.

4

تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةً

Ziingie katika Moto unao waka -

5

تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ آنِيَةٍ

Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.

6

لَيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِنْ ضَرِيعٍ

Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.

7

لَا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِي مِنْ جُوعٍ

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

8

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَاعِمَةٌ

Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.

9

لِسَعْيِهَا رَاضِيَةٌ

Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,

10

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ

Katika Bustani ya juu.

11

لَا تَسْمَعُ فِيهَا لَاغِيَةً

Hawatasikia humo upuuzi.

12

فِيهَا عَيْنٌ جَارِيَةٌ

Humo imo chemchem inayo miminika.

13

فِيهَا سُرُرٌ مَرْفُوعَةٌ

Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,

14

وَأَكْوَابٌ مَوْضُوعَةٌ

Na bilauri zilizo pangwa,

15

وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌ

Na matakia safu safu,

16

وَزَرَابِيُّ مَبْثُوثَةٌ

Na mazulia yaliyo tandikwa.

17

أَفَلَا يَنْظُرُونَ إِلَى الْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ

Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?

18

وَإِلَى السَّمَاءِ كَيْفَ رُفِعَتْ

Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?

19

وَإِلَى الْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ

Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?

20

وَإِلَى الْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ

Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?

21

فَذَكِّرْ إِنَّمَا أَنْتَ مُذَكِّرٌ

Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.

22

لَسْتَ عَلَيْهِمْ بِمُصَيْطِرٍ

Wewe si mwenye kuwatawalia.

23

إِلَّا مَنْ تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ

Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,

24

فَيُعَذِّبُهُ اللَّهُ الْعَذَابَ الْأَكْبَرَ

Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!

25

إِنَّ إِلَيْنَا إِيَابَهُمْ

Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.

26

ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُمْ

Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!

Islamic Vault

Quran Explorer

Ünlü okuyuculardan çoklu tercümeler, transliterasyonlar ve sesli tilavetlerle Kuran-ı Kerim'i okumak ve incelemek için kapsamlı bir çevrimiçi kaynak.

İşte bu, kendisinde şüphe olmayan kitaptır; Allah'a karşı gelmekten sakınanlar için bir yol göstericidir.

Kuran 2:2

Özellikler

  • Sesli Tilavetler
  • Çoklu Tercümeler
  • Transliterasyonlar
  • 114 Sure
  • 6.236 Ayet

© 2026 İslami Hazine. Tüm hakları saklıdır.

Allah'ın Kitabına saygı ve özenle yapılmıştır

Geliştiren Medita Development

Sorumluluk Reddi: Doğruluk için çaba göstersek de, lütfen önemli dini bilgileri güvenilir İslami alimler ve kaynaklarla doğrulayın. Bu platform eğitim amaçlıdır.