Islamic Vault

Corán

89

Al-Fajr

سورة الفجر

The Dawn30 versículos Mequí

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ وَالْفَجْرِ

Naapa kwa alfajiri,

2

وَلَيَالٍ عَشْرٍ

Na kwa masiku kumi,

3

وَالشَّفْعِ وَالْوَتْرِ

Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,

4

وَاللَّيْلِ إِذَا يَسْرِ

Na kwa usiku unapo pita,

5

هَلْ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِذِي حِجْرٍ

Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?

6

أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ

Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?

7

إِرَمَ ذَاتِ الْعِمَادِ

Wa Iram, wenye majumba marefu?

8

الَّتِي لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِي الْبِلَادِ

Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?

9

وَثَمُودَ الَّذِينَ جَابُوا الصَّخْرَ بِالْوَادِ

Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?

10

وَفِرْعَوْنَ ذِي الْأَوْتَادِ

Na Firauni mwenye vigingi?

11

الَّذِينَ طَغَوْا فِي الْبِلَادِ

Ambao walifanya jeuri katika nchi?

12

فَأَكْثَرُوا فِيهَا الْفَسَادَ

Wakakithirisha humo ufisadi?

13

فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ

Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.

14

إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ

Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.

15

فَأَمَّا الْإِنْسَانُ إِذَا مَا ابْتَلَاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَنِ

Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!

16

وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلَاهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ

Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!

17

كَلَّا ۖ بَلْ لَا تُكْرِمُونَ الْيَتِيمَ

Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,

18

وَلَا تَحَاضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ

Wala hamhimizani kulisha masikini;

19

وَتَأْكُلُونَ التُّرَاثَ أَكْلًا لَمًّا

Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,

20

وَتُحِبُّونَ الْمَالَ حُبًّا جَمًّا

Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.

21

كَلَّا إِذَا دُكَّتِ الْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا

Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,

22

وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا

Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,

23

وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الْإِنْسَانُ وَأَنَّىٰ لَهُ الذِّكْرَىٰ

Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?

24

يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي

Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!

25

فَيَوْمَئِذٍ لَا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ

Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.

26

وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌ

Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.

27

يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ

Ewe nafsi iliyo tua!

28

ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَرْضِيَّةً

Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.

29

فَادْخُلِي فِي عِبَادِي

Basi ingia miongoni mwa waja wangu,

30

وَادْخُلِي جَنَّتِي

Na ingia katika Pepo yangu.

Islamic Vault

Quran Explorer

Un recurso en línea completo para leer y estudiar el Sagrado Corán con múltiples traducciones, transliteraciones y recitaciones de audio de recitadores reconocidos.

Este es el Libro en el que no hay duda, una guía para los temerosos de Allah.

Corán 2:2

Características

  • Recitaciones de Audio
  • Múltiples Traducciones
  • Transliteraciones
  • 114 Suras
  • 6.236 Versículos

© 2026 Islamic Vault. Todos los derechos reservados.

Construido con reverencia y cuidado por el Libro de Allah

Desarrollado por Medita Development

Aviso legal: Aunque nos esforzamos por la precisión, por favor verifica la información religiosa importante con eruditos islámicos auténticos y fuentes confiables. Esta plataforma es con fines educativos.