Islamic Vault

Corán

88

Al-Ghaashiya

سورة الغاشية

The Overwhelming26 versículos Mequí

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ

Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?

2

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ خَاشِعَةٌ

Siku hiyo nyuso zitainama,

3

عَامِلَةٌ نَاصِبَةٌ

Zikifanya kazi, nazo taabani.

4

تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةً

Ziingie katika Moto unao waka -

5

تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ آنِيَةٍ

Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.

6

لَيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِنْ ضَرِيعٍ

Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.

7

لَا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِي مِنْ جُوعٍ

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

8

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَاعِمَةٌ

Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.

9

لِسَعْيِهَا رَاضِيَةٌ

Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,

10

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ

Katika Bustani ya juu.

11

لَا تَسْمَعُ فِيهَا لَاغِيَةً

Hawatasikia humo upuuzi.

12

فِيهَا عَيْنٌ جَارِيَةٌ

Humo imo chemchem inayo miminika.

13

فِيهَا سُرُرٌ مَرْفُوعَةٌ

Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,

14

وَأَكْوَابٌ مَوْضُوعَةٌ

Na bilauri zilizo pangwa,

15

وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌ

Na matakia safu safu,

16

وَزَرَابِيُّ مَبْثُوثَةٌ

Na mazulia yaliyo tandikwa.

17

أَفَلَا يَنْظُرُونَ إِلَى الْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ

Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?

18

وَإِلَى السَّمَاءِ كَيْفَ رُفِعَتْ

Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?

19

وَإِلَى الْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ

Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?

20

وَإِلَى الْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ

Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?

21

فَذَكِّرْ إِنَّمَا أَنْتَ مُذَكِّرٌ

Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.

22

لَسْتَ عَلَيْهِمْ بِمُصَيْطِرٍ

Wewe si mwenye kuwatawalia.

23

إِلَّا مَنْ تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ

Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,

24

فَيُعَذِّبُهُ اللَّهُ الْعَذَابَ الْأَكْبَرَ

Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!

25

إِنَّ إِلَيْنَا إِيَابَهُمْ

Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.

26

ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُمْ

Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!

Islamic Vault

Quran Explorer

Un recurso en línea completo para leer y estudiar el Sagrado Corán con múltiples traducciones, transliteraciones y recitaciones de audio de recitadores reconocidos.

Este es el Libro en el que no hay duda, una guía para los temerosos de Allah.

Corán 2:2

Características

  • Recitaciones de Audio
  • Múltiples Traducciones
  • Transliteraciones
  • 114 Suras
  • 6.236 Versículos

© 2026 Islamic Vault. Todos los derechos reservados.

Construido con reverencia y cuidado por el Libro de Allah

Desarrollado por Medita Development

Aviso legal: Aunque nos esforzamos por la precisión, por favor verifica la información religiosa importante con eruditos islámicos auténticos y fuentes confiables. Esta plataforma es con fines educativos.

Surah Al-Ghaashiya - Ali Muhsin Al-Barwani Swahili Translation | Islamic Vault | Islamic Vault