بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ الْقَارِعَةُ
Inayo gonga!
سورة القارعة
The Calamity • 11 verses • Meccan
Translated by Ali Muhsin Al-Barwani
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ الْقَارِعَةُ
Inayo gonga!
مَا الْقَارِعَةُ
Nini Inayo gonga?
وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْقَارِعَةُ
Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
يَوْمَ يَكُونُ النَّاسُ كَالْفَرَاشِ الْمَبْثُوثِ
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
وَتَكُونُ الْجِبَالُ كَالْعِهْنِ الْمَنْفُوشِ
Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
فَأَمَّا مَنْ ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
فَهُوَ فِي عِيشَةٍ رَاضِيَةٍ
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
وَأَمَّا مَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ
Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
فَأُمُّهُ هَاوِيَةٌ
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
وَمَا أَدْرَاكَ مَا هِيَهْ
Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
نَارٌ حَامِيَةٌ
Ni Moto mkali!