伊斯兰宝库

古兰经

85

Al-Burooj

سورة البروج

The Constellations22节经文 麦加章

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الْبُرُوجِ

Naapa kwa mbingu yenye Buruji!

2

وَالْيَوْمِ الْمَوْعُودِ

Na kwa siku iliyo ahidiwa!

3

وَشَاهِدٍ وَمَشْهُودٍ

Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!

4

قُتِلَ أَصْحَابُ الْأُخْدُودِ

Wameangamizwa watu wa makhandaki

5

النَّارِ ذَاتِ الْوَقُودِ

Yenye moto wenye kuni nyingi,

6

إِذْ هُمْ عَلَيْهَا قُعُودٌ

Walipo kuwa wamekaa hapo,

7

وَهُمْ عَلَىٰ مَا يَفْعَلُونَ بِالْمُؤْمِنِينَ شُهُودٌ

Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.

8

وَمَا نَقَمُوا مِنْهُمْ إِلَّا أَنْ يُؤْمِنُوا بِاللَّهِ الْعَزِيزِ الْحَمِيدِ

Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,

9

الَّذِي لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ وَاللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدٌ

Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.

10

إِنَّ الَّذِينَ فَتَنُوا الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ ثُمَّ لَمْ يَتُوبُوا فَلَهُمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمْ عَذَابُ الْحَرِيقِ

Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.

11

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَهُمْ جَنَّاتٌ تَجْرِي مِنْ تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ۚ ذَٰلِكَ الْفَوْزُ الْكَبِيرُ

Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

12

إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ

Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.

13

إِنَّهُ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ

Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,

14

وَهُوَ الْغَفُورُ الْوَدُودُ

Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,

15

ذُو الْعَرْشِ الْمَجِيدُ

Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,

16

فَعَّالٌ لِمَا يُرِيدُ

Atendaye ayatakayo.

17

هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْجُنُودِ

Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?

18

فِرْعَوْنَ وَثَمُودَ

Ya Firauni na Thamudi?

19

بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا فِي تَكْذِيبٍ

Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.

20

وَاللَّهُ مِنْ وَرَائِهِمْ مُحِيطٌ

Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.

21

بَلْ هُوَ قُرْآنٌ مَجِيدٌ

Bali hii ni Qur'ani tukufu

22

فِي لَوْحٍ مَحْفُوظٍ

Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.

Islamic Vault

Quran Explorer

一个全面的在线资源,用于阅读和学习神圣古兰经,提供多种翻译、音译和著名诵读者的音频诵读。

这部经典,其中毫无可疑,是敬畏者的向导。

古兰经 2:2

功能

  • 音频诵读
  • 多种翻译
  • 音译
  • 114章
  • 6,236节经文

© 2026 伊斯兰宝库。保留所有权利。

以对真主之书的敬畏和关怀而构建

免责声明: 虽然我们力求准确,但请与可靠的伊斯兰学者和来源核实重要的宗教信息。本平台仅供教育目的。