伊斯兰宝库

古兰经

84

Al-Inshiqaaq

سورة الإنشقاق

The Splitting Open25节经文 麦加章

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ إِذَا السَّمَاءُ انْشَقَّتْ

Itapo chanika mbingu,

2

وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

3

وَإِذَا الْأَرْضُ مُدَّتْ

Na ardhi itakapo tanuliwa,

4

وَأَلْقَتْ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتْ

Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,

5

وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

6

يَا أَيُّهَا الْإِنْسَانُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدْحًا فَمُلَاقِيهِ

Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.

7

فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ

Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,

8

فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًا يَسِيرًا

Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,

9

وَيَنْقَلِبُ إِلَىٰ أَهْلِهِ مَسْرُورًا

Na arudi kwa ahali zake na furaha.

10

وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ وَرَاءَ ظَهْرِهِ

Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,

11

فَسَوْفَ يَدْعُو ثُبُورًا

Basi huyo ataomba kuteketea.

12

وَيَصْلَىٰ سَعِيرًا

Na ataingia Motoni.

13

إِنَّهُ كَانَ فِي أَهْلِهِ مَسْرُورًا

Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.

14

إِنَّهُ ظَنَّ أَنْ لَنْ يَحُورَ

Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.

15

بَلَىٰ إِنَّ رَبَّهُ كَانَ بِهِ بَصِيرًا

Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!

16

فَلَا أُقْسِمُ بِالشَّفَقِ

Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,

17

وَاللَّيْلِ وَمَا وَسَقَ

Na kwa usiku na unavyo vikusanya,

18

وَالْقَمَرِ إِذَا اتَّسَقَ

Na kwa mwezi unapo pevuka,

19

لَتَرْكَبُنَّ طَبَقًا عَنْ طَبَقٍ

Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!

20

فَمَا لَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ

Basi wana nini hawaamini?

21

وَإِذَا قُرِئَ عَلَيْهِمُ الْقُرْآنُ لَا يَسْجُدُونَ ۩

Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?

22

بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا يُكَذِّبُونَ

Bali walio kufuru wanakanusha tu.

23

وَاللَّهُ أَعْلَمُ بِمَا يُوعُونَ

Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.

24

فَبَشِّرْهُمْ بِعَذَابٍ أَلِيمٍ

Basi wabashirie adhabu chungu!

25

إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍ

Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.

Islamic Vault

Quran Explorer

一个全面的在线资源,用于阅读和学习神圣古兰经,提供多种翻译、音译和著名诵读者的音频诵读。

这部经典,其中毫无可疑,是敬畏者的向导。

古兰经 2:2

功能

  • 音频诵读
  • 多种翻译
  • 音译
  • 114章
  • 6,236节经文

© 2026 伊斯兰宝库。保留所有权利。

以对真主之书的敬畏和关怀而构建

免责声明: 虽然我们力求准确,但请与可靠的伊斯兰学者和来源核实重要的宗教信息。本平台仅供教育目的。