Islamic Vault
85

Al-Burooj

سورة البروج

The Constellations22 ayat Makkiyah

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الْبُرُوجِ

Naapa kwa mbingu yenye Buruji!

2

وَالْيَوْمِ الْمَوْعُودِ

Na kwa siku iliyo ahidiwa!

3

وَشَاهِدٍ وَمَشْهُودٍ

Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!

4

قُتِلَ أَصْحَابُ الْأُخْدُودِ

Wameangamizwa watu wa makhandaki

5

النَّارِ ذَاتِ الْوَقُودِ

Yenye moto wenye kuni nyingi,

6

إِذْ هُمْ عَلَيْهَا قُعُودٌ

Walipo kuwa wamekaa hapo,

7

وَهُمْ عَلَىٰ مَا يَفْعَلُونَ بِالْمُؤْمِنِينَ شُهُودٌ

Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.

8

وَمَا نَقَمُوا مِنْهُمْ إِلَّا أَنْ يُؤْمِنُوا بِاللَّهِ الْعَزِيزِ الْحَمِيدِ

Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,

9

الَّذِي لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ وَاللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدٌ

Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.

10

إِنَّ الَّذِينَ فَتَنُوا الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ ثُمَّ لَمْ يَتُوبُوا فَلَهُمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمْ عَذَابُ الْحَرِيقِ

Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.

11

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَهُمْ جَنَّاتٌ تَجْرِي مِنْ تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ۚ ذَٰلِكَ الْفَوْزُ الْكَبِيرُ

Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

12

إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ

Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.

13

إِنَّهُ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ

Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,

14

وَهُوَ الْغَفُورُ الْوَدُودُ

Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,

15

ذُو الْعَرْشِ الْمَجِيدُ

Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,

16

فَعَّالٌ لِمَا يُرِيدُ

Atendaye ayatakayo.

17

هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْجُنُودِ

Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?

18

فِرْعَوْنَ وَثَمُودَ

Ya Firauni na Thamudi?

19

بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا فِي تَكْذِيبٍ

Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.

20

وَاللَّهُ مِنْ وَرَائِهِمْ مُحِيطٌ

Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.

21

بَلْ هُوَ قُرْآنٌ مَجِيدٌ

Bali hii ni Qur'ani tukufu

22

فِي لَوْحٍ مَحْفُوظٍ

Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.

Islamic Vault

Quran Explorer

Sumber online lengkap untuk membaca dan mempelajari Al-Quran dengan berbagai terjemahan, transliterasi, dan tilawah dari qari terkenal.

Kitab ini tidak ada keraguan padanya; petunjuk bagi mereka yang bertakwa.

Al-Quran 2:2

Fitur

  • Tilawah Audio
  • Berbagai Terjemahan
  • Transliterasi
  • 114 Surah
  • 6.236 Ayat

© 2026 Islamic Vault. Hak cipta dilindungi.

Dibuat dengan penghormatan dan kehati-hatian untuk Kitabullah

Dikembangkan oleh Medita Development

Penyangkalan: Meskipun kami berusaha untuk akurat, mohon verifikasi informasi agama penting dengan ulama Islam dan sumber terpercaya. Platform ini untuk tujuan pendidikan.