Islamic Vault
84

Al-Inshiqaaq

سورة الإنشقاق

The Splitting Open25 ayat Makkiyah

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ إِذَا السَّمَاءُ انْشَقَّتْ

Itapo chanika mbingu,

2

وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

3

وَإِذَا الْأَرْضُ مُدَّتْ

Na ardhi itakapo tanuliwa,

4

وَأَلْقَتْ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتْ

Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,

5

وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

6

يَا أَيُّهَا الْإِنْسَانُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدْحًا فَمُلَاقِيهِ

Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.

7

فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ

Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,

8

فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًا يَسِيرًا

Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,

9

وَيَنْقَلِبُ إِلَىٰ أَهْلِهِ مَسْرُورًا

Na arudi kwa ahali zake na furaha.

10

وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ وَرَاءَ ظَهْرِهِ

Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,

11

فَسَوْفَ يَدْعُو ثُبُورًا

Basi huyo ataomba kuteketea.

12

وَيَصْلَىٰ سَعِيرًا

Na ataingia Motoni.

13

إِنَّهُ كَانَ فِي أَهْلِهِ مَسْرُورًا

Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.

14

إِنَّهُ ظَنَّ أَنْ لَنْ يَحُورَ

Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.

15

بَلَىٰ إِنَّ رَبَّهُ كَانَ بِهِ بَصِيرًا

Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!

16

فَلَا أُقْسِمُ بِالشَّفَقِ

Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,

17

وَاللَّيْلِ وَمَا وَسَقَ

Na kwa usiku na unavyo vikusanya,

18

وَالْقَمَرِ إِذَا اتَّسَقَ

Na kwa mwezi unapo pevuka,

19

لَتَرْكَبُنَّ طَبَقًا عَنْ طَبَقٍ

Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!

20

فَمَا لَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ

Basi wana nini hawaamini?

21

وَإِذَا قُرِئَ عَلَيْهِمُ الْقُرْآنُ لَا يَسْجُدُونَ ۩

Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?

22

بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا يُكَذِّبُونَ

Bali walio kufuru wanakanusha tu.

23

وَاللَّهُ أَعْلَمُ بِمَا يُوعُونَ

Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.

24

فَبَشِّرْهُمْ بِعَذَابٍ أَلِيمٍ

Basi wabashirie adhabu chungu!

25

إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍ

Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.

Islamic Vault

Quran Explorer

Sumber online lengkap untuk membaca dan mempelajari Al-Quran dengan berbagai terjemahan, transliterasi, dan tilawah dari qari terkenal.

Kitab ini tidak ada keraguan padanya; petunjuk bagi mereka yang bertakwa.

Al-Quran 2:2

Fitur

  • Tilawah Audio
  • Berbagai Terjemahan
  • Transliterasi
  • 114 Surah
  • 6.236 Ayat

© 2026 Islamic Vault. Hak cipta dilindungi.

Dibuat dengan penghormatan dan kehati-hatian untuk Kitabullah

Dikembangkan oleh Medita Development

Penyangkalan: Meskipun kami berusaha untuk akurat, mohon verifikasi informasi agama penting dengan ulama Islam dan sumber terpercaya. Platform ini untuk tujuan pendidikan.