伊斯兰宝库

古兰经

81

At-Takwir

سورة التكوير

The Overthrowing29节经文 麦加章

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ إِذَا الشَّمْسُ كُوِّرَتْ

Jua litakapo kunjwa,

2

وَإِذَا النُّجُومُ انْكَدَرَتْ

Na nyota zikazimwa,

3

وَإِذَا الْجِبَالُ سُيِّرَتْ

Na milima ikaondolewa,

4

وَإِذَا الْعِشَارُ عُطِّلَتْ

Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,

5

وَإِذَا الْوُحُوشُ حُشِرَتْ

Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,

6

وَإِذَا الْبِحَارُ سُجِّرَتْ

Na bahari zikawaka moto,

7

وَإِذَا النُّفُوسُ زُوِّجَتْ

Na nafsi zikaunganishwa,

8

وَإِذَا الْمَوْءُودَةُ سُئِلَتْ

Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,

9

بِأَيِّ ذَنْبٍ قُتِلَتْ

Kwa kosa gani aliuliwa?

10

وَإِذَا الصُّحُفُ نُشِرَتْ

Na madaftari yatakapo enezwa,

11

وَإِذَا السَّمَاءُ كُشِطَتْ

Na mbingu itapo tanduliwa,

12

وَإِذَا الْجَحِيمُ سُعِّرَتْ

Na Jahannamu itapo chochewa,

13

وَإِذَا الْجَنَّةُ أُزْلِفَتْ

Na Pepo ikasogezwa,

14

عَلِمَتْ نَفْسٌ مَا أَحْضَرَتْ

Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.

15

فَلَا أُقْسِمُ بِالْخُنَّسِ

Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,

16

الْجَوَارِ الْكُنَّسِ

Zinazo kwenda, kisha zikajificha,

17

وَاللَّيْلِ إِذَا عَسْعَسَ

Na kwa usiku unapo pungua,

18

وَالصُّبْحِ إِذَا تَنَفَّسَ

Na kwa asubuhi inapo pambazuka,

19

إِنَّهُ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ

Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,

20

ذِي قُوَّةٍ عِنْدَ ذِي الْعَرْشِ مَكِينٍ

Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,

21

مُطَاعٍ ثَمَّ أَمِينٍ

Anaye t'iiwa, tena muaminifu.

22

وَمَا صَاحِبُكُمْ بِمَجْنُونٍ

Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.

23

وَلَقَدْ رَآهُ بِالْأُفُقِ الْمُبِينِ

Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.

24

وَمَا هُوَ عَلَى الْغَيْبِ بِضَنِينٍ

Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.

25

وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَيْطَانٍ رَجِيمٍ

Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.

26

فَأَيْنَ تَذْهَبُونَ

Basi mnakwenda wapi?

27

إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِلْعَالَمِينَ

Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

28

لِمَنْ شَاءَ مِنْكُمْ أَنْ يَسْتَقِيمَ

Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.

29

وَمَا تَشَاءُونَ إِلَّا أَنْ يَشَاءَ اللَّهُ رَبُّ الْعَالَمِينَ

Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Islamic Vault

Quran Explorer

一个全面的在线资源,用于阅读和学习神圣古兰经,提供多种翻译、音译和著名诵读者的音频诵读。

这部经典,其中毫无可疑,是敬畏者的向导。

古兰经 2:2

功能

  • 音频诵读
  • 多种翻译
  • 音译
  • 114章
  • 6,236节经文

© 2026 伊斯兰宝库。保留所有权利。

以对真主之书的敬畏和关怀而构建

免责声明: 虽然我们力求准确,但请与可靠的伊斯兰学者和来源核实重要的宗教信息。本平台仅供教育目的。