伊斯兰宝库

古兰经

75

Al-Qiyaama

سورة القيامة

The Resurrection40节经文 麦加章

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ لَا أُقْسِمُ بِيَوْمِ الْقِيَامَةِ

Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!

2

وَلَا أُقْسِمُ بِالنَّفْسِ اللَّوَّامَةِ

Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!

3

أَيَحْسَبُ الْإِنْسَانُ أَلَّنْ نَجْمَعَ عِظَامَهُ

Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?

4

بَلَىٰ قَادِرِينَ عَلَىٰ أَنْ نُسَوِّيَ بَنَانَهُ

Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!

5

بَلْ يُرِيدُ الْإِنْسَانُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُ

Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.

6

يَسْأَلُ أَيَّانَ يَوْمُ الْقِيَامَةِ

Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?

7

فَإِذَا بَرِقَ الْبَصَرُ

Basi jicho litapo dawaa,

8

وَخَسَفَ الْقَمَرُ

Na mwezi utapo patwa,

9

وَجُمِعَ الشَّمْسُ وَالْقَمَرُ

Na likakusanywa jua na mwezi,

10

يَقُولُ الْإِنْسَانُ يَوْمَئِذٍ أَيْنَ الْمَفَرُّ

Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?

11

كَلَّا لَا وَزَرَ

La! Hapana pa kukimbilia!

12

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ الْمُسْتَقَرُّ

Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.

13

يُنَبَّأُ الْإِنْسَانُ يَوْمَئِذٍ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ

Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.

14

بَلِ الْإِنْسَانُ عَلَىٰ نَفْسِهِ بَصِيرَةٌ

Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.

15

وَلَوْ أَلْقَىٰ مَعَاذِيرَهُ

Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.

16

لَا تُحَرِّكْ بِهِ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِ

Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.

17

إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُ وَقُرْآنَهُ

Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.

18

فَإِذَا قَرَأْنَاهُ فَاتَّبِعْ قُرْآنَهُ

Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.

19

ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُ

Kisha ni juu yetu kuubainisha.

20

كَلَّا بَلْ تُحِبُّونَ الْعَاجِلَةَ

Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,

21

وَتَذَرُونَ الْآخِرَةَ

Na mnaacha maisha ya Akhera.

22

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَاضِرَةٌ

Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,

23

إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٌ

Zinamwangallia Mola wao Mlezi.

24

وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ بَاسِرَةٌ

Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.

25

تَظُنُّ أَنْ يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَةٌ

Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.

26

كَلَّا إِذَا بَلَغَتِ التَّرَاقِيَ

La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,

27

وَقِيلَ مَنْ ۜ رَاقٍ

Na pakasemwa: Nani wa kumganga?

28

وَظَنَّ أَنَّهُ الْفِرَاقُ

Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;

29

وَالْتَفَّتِ السَّاقُ بِالسَّاقِ

Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,

30

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ الْمَسَاقُ

Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!

31

فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ

Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.

32

وَلَٰكِنْ كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ

Bali alikanusha, na akageuka.

33

ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰ أَهْلِهِ يَتَمَطَّىٰ

Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.

34

أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ

Ole wako, ole wako!

35

ثُمَّ أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ

Kisha Ole wako, ole wako!

36

أَيَحْسَبُ الْإِنْسَانُ أَنْ يُتْرَكَ سُدًى

Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?

37

أَلَمْ يَكُ نُطْفَةً مِنْ مَنِيٍّ يُمْنَىٰ

Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?

38

ثُمَّ كَانَ عَلَقَةً فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ

Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.

39

فَجَعَلَ مِنْهُ الزَّوْجَيْنِ الذَّكَرَ وَالْأُنْثَىٰ

Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.

40

أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَنْ يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ

Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?

Islamic Vault

Quran Explorer

一个全面的在线资源,用于阅读和学习神圣古兰经,提供多种翻译、音译和著名诵读者的音频诵读。

这部经典,其中毫无可疑,是敬畏者的向导。

古兰经 2:2

功能

  • 音频诵读
  • 多种翻译
  • 音译
  • 114章
  • 6,236节经文

© 2026 伊斯兰宝库。保留所有权利。

以对真主之书的敬畏和关怀而构建

免责声明: 虽然我们力求准确,但请与可靠的伊斯兰学者和来源核实重要的宗教信息。本平台仅供教育目的。