伊斯兰宝库

古兰经

69

Al-Haaqqa

سورة الحاقة

The Reality52节经文 麦加章

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ الْحَاقَّةُ

Tukio la haki.

2

مَا الْحَاقَّةُ

Nini hilo Tukio la haki?

3

وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْحَاقَّةُ

Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?

4

كَذَّبَتْ ثَمُودُ وَعَادٌ بِالْقَارِعَةِ

Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.

5

فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهْلِكُوا بِالطَّاغِيَةِ

Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.

6

وَأَمَّا عَادٌ فَأُهْلِكُوا بِرِيحٍ صَرْصَرٍ عَاتِيَةٍ

Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.

7

سَخَّرَهَا عَلَيْهِمْ سَبْعَ لَيَالٍ وَثَمَانِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومًا فَتَرَى الْقَوْمَ فِيهَا صَرْعَىٰ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ خَاوِيَةٍ

Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.

8

فَهَلْ تَرَىٰ لَهُمْ مِنْ بَاقِيَةٍ

Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?

9

وَجَاءَ فِرْعَوْنُ وَمَنْ قَبْلَهُ وَالْمُؤْتَفِكَاتُ بِالْخَاطِئَةِ

Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.

10

فَعَصَوْا رَسُولَ رَبِّهِمْ فَأَخَذَهُمْ أَخْذَةً رَابِيَةً

Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.

11

إِنَّا لَمَّا طَغَى الْمَاءُ حَمَلْنَاكُمْ فِي الْجَارِيَةِ

Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,

12

لِنَجْعَلَهَا لَكُمْ تَذْكِرَةً وَتَعِيَهَا أُذُنٌ وَاعِيَةٌ

Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.

13

فَإِذَا نُفِخَ فِي الصُّورِ نَفْخَةٌ وَاحِدَةٌ

Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,

14

وَحُمِلَتِ الْأَرْضُ وَالْجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةً وَاحِدَةً

Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,

15

فَيَوْمَئِذٍ وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ

Siku hiyo ndio Tukio litatukia.

16

وَانْشَقَّتِ السَّمَاءُ فَهِيَ يَوْمَئِذٍ وَاهِيَةٌ

Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.

17

وَالْمَلَكُ عَلَىٰ أَرْجَائِهَا ۚ وَيَحْمِلُ عَرْشَ رَبِّكَ فَوْقَهُمْ يَوْمَئِذٍ ثَمَانِيَةٌ

Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.

18

يَوْمَئِذٍ تُعْرَضُونَ لَا تَخْفَىٰ مِنْكُمْ خَافِيَةٌ

Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.

19

فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ فَيَقُولُ هَاؤُمُ اقْرَءُوا كِتَابِيَهْ

Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!

20

إِنِّي ظَنَنْتُ أَنِّي مُلَاقٍ حِسَابِيَهْ

Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.

21

فَهُوَ فِي عِيشَةٍ رَاضِيَةٍ

Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,

22

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ

Katika Bustani ya juu,

23

قُطُوفُهَا دَانِيَةٌ

Matunda yake yakaribu.

24

كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا أَسْلَفْتُمْ فِي الْأَيَّامِ الْخَالِيَةِ

Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.

25

وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِشِمَالِهِ فَيَقُولُ يَا لَيْتَنِي لَمْ أُوتَ كِتَابِيَهْ

Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!

26

وَلَمْ أَدْرِ مَا حِسَابِيَهْ

Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.

27

يَا لَيْتَهَا كَانَتِ الْقَاضِيَةَ

Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.

28

مَا أَغْنَىٰ عَنِّي مَالِيَهْ ۜ

Mali yangu hayakunifaa kitu.

29

هَلَكَ عَنِّي سُلْطَانِيَهْ

Madaraka yangu yamenipotea.

30

خُذُوهُ فَغُلُّوهُ

(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!

31

ثُمَّ الْجَحِيمَ صَلُّوهُ

Kisha mtupeni Motoni!

32

ثُمَّ فِي سِلْسِلَةٍ ذَرْعُهَا سَبْعُونَ ذِرَاعًا فَاسْلُكُوهُ

Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!

33

إِنَّهُ كَانَ لَا يُؤْمِنُ بِاللَّهِ الْعَظِيمِ

Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,

34

وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ

Wala hahimizi kulisha masikini.

35

فَلَيْسَ لَهُ الْيَوْمَ هَاهُنَا حَمِيمٌ

Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,

36

وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنْ غِسْلِينٍ

Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.

37

لَا يَأْكُلُهُ إِلَّا الْخَاطِئُونَ

Chakula hicho hawakili ila wakosefu.

38

فَلَا أُقْسِمُ بِمَا تُبْصِرُونَ

Basi naapa kwa mnavyo viona,

39

وَمَا لَا تُبْصِرُونَ

Na msivyo viona,

40

إِنَّهُ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ

Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.

41

وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَاعِرٍ ۚ قَلِيلًا مَا تُؤْمِنُونَ

Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.

42

وَلَا بِقَوْلِ كَاهِنٍ ۚ قَلِيلًا مَا تَذَكَّرُونَ

Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.

43

تَنْزِيلٌ مِنْ رَبِّ الْعَالَمِينَ

Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

44

وَلَوْ تَقَوَّلَ عَلَيْنَا بَعْضَ الْأَقَاوِيلِ

Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,

45

لَأَخَذْنَا مِنْهُ بِالْيَمِينِ

Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,

46

ثُمَّ لَقَطَعْنَا مِنْهُ الْوَتِينَ

Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!

47

فَمَا مِنْكُمْ مِنْ أَحَدٍ عَنْهُ حَاجِزِينَ

Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.

48

وَإِنَّهُ لَتَذْكِرَةٌ لِلْمُتَّقِينَ

Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.

49

وَإِنَّا لَنَعْلَمُ أَنَّ مِنْكُمْ مُكَذِّبِينَ

Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.

50

وَإِنَّهُ لَحَسْرَةٌ عَلَى الْكَافِرِينَ

Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.

51

وَإِنَّهُ لَحَقُّ الْيَقِينِ

Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.

52

فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.

Islamic Vault

Quran Explorer

一个全面的在线资源,用于阅读和学习神圣古兰经,提供多种翻译、音译和著名诵读者的音频诵读。

这部经典,其中毫无可疑,是敬畏者的向导。

古兰经 2:2

功能

  • 音频诵读
  • 多种翻译
  • 音译
  • 114章
  • 6,236节经文

© 2026 伊斯兰宝库。保留所有权利。

以对真主之书的敬畏和关怀而构建

免责声明: 虽然我们力求准确,但请与可靠的伊斯兰学者和来源核实重要的宗教信息。本平台仅供教育目的。