100

Al-Aadiyaat

سورة العاديات

The Chargers11 ayet Mekki

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ وَالْعَادِيَاتِ ضَبْحًا

Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,

2

فَالْمُورِيَاتِ قَدْحًا

Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,

3

فَالْمُغِيرَاتِ صُبْحًا

Wakishambulia wakati wa asubuhi,

4

فَأَثَرْنَ بِهِ نَقْعًا

Huku wakitimua vumbi,

5

فَوَسَطْنَ بِهِ جَمْعًا

Na wakijitoma kati ya kundi,

6

إِنَّ الْإِنْسَانَ لِرَبِّهِ لَكَنُودٌ

Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!

7

وَإِنَّهُ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٌ

Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!

8

وَإِنَّهُ لِحُبِّ الْخَيْرِ لَشَدِيدٌ

Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!

9

۞ أَفَلَا يَعْلَمُ إِذَا بُعْثِرَ مَا فِي الْقُبُورِ

Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?

10

وَحُصِّلَ مَا فِي الصُّدُورِ

Na yakakusanywa yaliomo vifuani?

11

إِنَّ رَبَّهُمْ بِهِمْ يَوْمَئِذٍ لَخَبِيرٌ

Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!