93

Ad-Dhuhaa

سورة الضحى

The Morning Hours11 ayat Makkiyyah

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ وَالضُّحَىٰ

Naapa kwa mchana!

2

وَاللَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ

Na kwa usiku unapo tanda!

3

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ

Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.

4

وَلَلْآخِرَةُ خَيْرٌ لَكَ مِنَ الْأُولَىٰ

Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.

5

وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰ

Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.

6

أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًا فَآوَىٰ

Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?

7

وَوَجَدَكَ ضَالًّا فَهَدَىٰ

Na akakukuta umepotea akakuongoa?

8

وَوَجَدَكَ عَائِلًا فَأَغْنَىٰ

Akakukuta mhitaji akakutosheleza?

9

فَأَمَّا الْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ

Basi yatima usimwonee!

10

وَأَمَّا السَّائِلَ فَلَا تَنْهَرْ

Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!

11

وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ

Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.