Islamic Vault

Quran

90

Al-Balad

سورة البلد

The City20 ayat Makkiyyah

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ لَا أُقْسِمُ بِهَٰذَا الْبَلَدِ

Naapa kwa Mji huu!

2

وَأَنْتَ حِلٌّ بِهَٰذَا الْبَلَدِ

Nawe unaukaa Mji huu.

3

وَوَالِدٍ وَمَا وَلَدَ

Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.

4

لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنْسَانَ فِي كَبَدٍ

Hakika tumemuumba mtu katika taabu.

5

أَيَحْسَبُ أَنْ لَنْ يَقْدِرَ عَلَيْهِ أَحَدٌ

Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?

6

يَقُولُ أَهْلَكْتُ مَالًا لُبَدًا

Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.

7

أَيَحْسَبُ أَنْ لَمْ يَرَهُ أَحَدٌ

Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?

8

أَلَمْ نَجْعَلْ لَهُ عَيْنَيْنِ

Kwani hatukumpa macho mawili?

9

وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ

Na ulimi, na midomo miwili?

10

وَهَدَيْنَاهُ النَّجْدَيْنِ

Na tukambainishia zote njia mbili?

11

فَلَا اقْتَحَمَ الْعَقَبَةَ

Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

12

وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْعَقَبَةُ

Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?

13

فَكُّ رَقَبَةٍ

Kumkomboa mtumwa;

14

أَوْ إِطْعَامٌ فِي يَوْمٍ ذِي مَسْغَبَةٍ

Au kumlisha siku ya njaa

15

يَتِيمًا ذَا مَقْرَبَةٍ

Yatima aliye jamaa,

16

أَوْ مِسْكِينًا ذَا مَتْرَبَةٍ

Au masikini aliye vumbini.

17

ثُمَّ كَانَ مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ وَتَوَاصَوْا بِالْمَرْحَمَةِ

Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.

18

أُولَٰئِكَ أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ

Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.

19

وَالَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِنَا هُمْ أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ

Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.

20

عَلَيْهِمْ نَارٌ مُؤْصَدَةٌ

Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.

Islamic Vault

Quran Explorer

Sumber dalam talian yang komprehensif untuk membaca dan mengkaji Al-Quran dengan pelbagai terjemahan, transliterasi, dan bacaan audio daripada qari terkenal.

Kitab ini tidak ada keraguan padanya, petunjuk bagi orang-orang yang bertakwa.

Al-Quran 2:2

Ciri-ciri

  • Bacaan Audio
  • Pelbagai Terjemahan
  • Transliterasi
  • 114 Surah
  • 6,236 Ayat

© 2026 Islamic Vault. Hak cipta terpelihara.

Dibina dengan penghormatan dan ketelitian untuk Kitabullah

Dibangunkan oleh Medita Development

Penafian: Walaupun kami berusaha untuk ketepatan, sila sahkan maklumat agama penting dengan ulama Islam dan sumber yang sahih. Platform ini adalah untuk tujuan pendidikan.