بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ وَالشَّمْسِ وَضُحَاهَا
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
سورة الشمس
The Sun • 15 ayat • Makkiyah
Translated by Ali Muhsin Al-Barwani
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ وَالشَّمْسِ وَضُحَاهَا
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
وَالْقَمَرِ إِذَا تَلَاهَا
Na kwa mwezi unapo lifuatia!
وَالنَّهَارِ إِذَا جَلَّاهَا
Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
وَاللَّيْلِ إِذَا يَغْشَاهَا
Na kwa usiku unapo lifunika!
وَالسَّمَاءِ وَمَا بَنَاهَا
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
وَالْأَرْضِ وَمَا طَحَاهَا
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
وَنَفْسٍ وَمَا سَوَّاهَا
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَاهَا
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
قَدْ أَفْلَحَ مَنْ زَكَّاهَا
Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
وَقَدْ خَابَ مَنْ دَسَّاهَا
Na hakika amekhasiri aliye iviza.
كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِطَغْوَاهَا
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
إِذِ انْبَعَثَ أَشْقَاهَا
Alipo simama mwovu wao mkubwa,
فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ اللَّهِ نَاقَةَ اللَّهِ وَسُقْيَاهَا
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمْدَمَ عَلَيْهِمْ رَبُّهُمْ بِذَنْبِهِمْ فَسَوَّاهَا
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
وَلَا يَخَافُ عُقْبَاهَا
Wala Yeye haogopi matokeo yake.