Islamic Vault

Quran

77

Al-Mursalaat

سورة المرسلات

The Emissaries50 ayat Makkiyah

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ وَالْمُرْسَلَاتِ عُرْفًا

Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!

2

فَالْعَاصِفَاتِ عَصْفًا

Na zinazo vuma kwa kasi!

3

وَالنَّاشِرَاتِ نَشْرًا

Na zikaeneza maeneo yote!

4

فَالْفَارِقَاتِ فَرْقًا

Na zinazo farikisha zikatawanya!

5

فَالْمُلْقِيَاتِ ذِكْرًا

Na zinazo peleka mawaidha!

6

عُذْرًا أَوْ نُذْرًا

Kwa kuudhuru au kuonya,

7

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَاقِعٌ

Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!

8

فَإِذَا النُّجُومُ طُمِسَتْ

Wakati nyota zitakapo futwa,

9

وَإِذَا السَّمَاءُ فُرِجَتْ

Na mbingu zitakapo pasuliwa,

10

وَإِذَا الْجِبَالُ نُسِفَتْ

Na milima itakapo peperushwa,

11

وَإِذَا الرُّسُلُ أُقِّتَتْ

Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,

12

لِأَيِّ يَوْمٍ أُجِّلَتْ

Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?

13

لِيَوْمِ الْفَصْلِ

Kwa siku ya kupambanua!

14

وَمَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الْفَصْلِ

Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?

15

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِلْمُكَذِّبِينَ

Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!

16

أَلَمْ نُهْلِكِ الْأَوَّلِينَ

Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?

17

ثُمَّ نُتْبِعُهُمُ الْآخِرِينَ

Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?

18

كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ

Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!

19

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِلْمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

20

أَلَمْ نَخْلُقْكُمْ مِنْ مَاءٍ مَهِينٍ

Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?

21

فَجَعَلْنَاهُ فِي قَرَارٍ مَكِينٍ

Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?

22

إِلَىٰ قَدَرٍ مَعْلُومٍ

Mpaka muda maalumu?

23

فَقَدَرْنَا فَنِعْمَ الْقَادِرُونَ

Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.

24

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِلْمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

25

أَلَمْ نَجْعَلِ الْأَرْضَ كِفَاتًا

Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya

26

أَحْيَاءً وَأَمْوَاتًا

Walio hai na maiti?

27

وَجَعَلْنَا فِيهَا رَوَاسِيَ شَامِخَاتٍ وَأَسْقَيْنَاكُمْ مَاءً فُرَاتًا

Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?

28

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِلْمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

29

انْطَلِقُوا إِلَىٰ مَا كُنْتُمْ بِهِ تُكَذِّبُونَ

Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!

30

انْطَلِقُوا إِلَىٰ ظِلٍّ ذِي ثَلَاثِ شُعَبٍ

Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!

31

لَا ظَلِيلٍ وَلَا يُغْنِي مِنَ اللَّهَبِ

Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.

32

إِنَّهَا تَرْمِي بِشَرَرٍ كَالْقَصْرِ

Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!

33

كَأَنَّهُ جِمَالَتٌ صُفْرٌ

Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!

34

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِلْمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

35

هَٰذَا يَوْمُ لَا يَنْطِقُونَ

Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,

36

وَلَا يُؤْذَنُ لَهُمْ فَيَعْتَذِرُونَ

Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.

37

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِلْمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

38

هَٰذَا يَوْمُ الْفَصْلِ ۖ جَمَعْنَاكُمْ وَالْأَوَّلِينَ

Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.

39

فَإِنْ كَانَ لَكُمْ كَيْدٌ فَكِيدُونِ

Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!

40

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِلْمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

41

إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي ظِلَالٍ وَعُيُونٍ

Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,

42

وَفَوَاكِهَ مِمَّا يَشْتَهُونَ

Na matunda wanayo yapenda,

43

كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا كُنْتُمْ تَعْمَلُونَ

Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.

44

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ

Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.

45

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِلْمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

46

كُلُوا وَتَمَتَّعُوا قَلِيلًا إِنَّكُمْ مُجْرِمُونَ

Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!

47

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِلْمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

48

وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ارْكَعُوا لَا يَرْكَعُونَ

Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.

49

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِلْمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

50

فَبِأَيِّ حَدِيثٍ بَعْدَهُ يُؤْمِنُونَ

Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?

Islamic Vault

Quran Explorer

Sumber online lengkap untuk membaca dan mempelajari Al-Quran dengan berbagai terjemahan, transliterasi, dan tilawah dari qari terkenal.

Kitab ini tidak ada keraguan padanya; petunjuk bagi mereka yang bertakwa.

Al-Quran 2:2

Fitur

  • Tilawah Audio
  • Berbagai Terjemahan
  • Transliterasi
  • 114 Surah
  • 6.236 Ayat

© 2026 Islamic Vault. Hak cipta dilindungi.

Dibuat dengan penghormatan dan kehati-hatian untuk Kitabullah

Dikembangkan oleh Medita Development

Penyangkalan: Meskipun kami berusaha untuk akurat, mohon verifikasi informasi agama penting dengan ulama Islam dan sumber terpercaya. Platform ini untuk tujuan pendidikan.