Islamic Vault
70

Al-Ma'aarij

سورة المعارج

The Ascending Stairways44 ayat Makkiyah

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ سَأَلَ سَائِلٌ بِعَذَابٍ وَاقِعٍ

Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,

2

لِلْكَافِرِينَ لَيْسَ لَهُ دَافِعٌ

Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -

3

مِنَ اللَّهِ ذِي الْمَعَارِجِ

Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.

4

تَعْرُجُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ إِلَيْهِ فِي يَوْمٍ كَانَ مِقْدَارُهُ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَةٍ

Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!

5

فَاصْبِرْ صَبْرًا جَمِيلًا

Basi subiri kwa subira njema.

6

إِنَّهُمْ يَرَوْنَهُ بَعِيدًا

Hakika wao wanaiona iko mbali,

7

وَنَرَاهُ قَرِيبًا

Na Sisi tunaiona iko karibu.

8

يَوْمَ تَكُونُ السَّمَاءُ كَالْمُهْلِ

Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.

9

وَتَكُونُ الْجِبَالُ كَالْعِهْنِ

Na milima itakuwa kama sufi.

10

وَلَا يَسْأَلُ حَمِيمٌ حَمِيمًا

Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.

11

يُبَصَّرُونَهُمْ ۚ يَوَدُّ الْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِي مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍ بِبَنِيهِ

Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,

12

وَصَاحِبَتِهِ وَأَخِيهِ

Na mkewe, na nduguye,

13

وَفَصِيلَتِهِ الَّتِي تُؤْوِيهِ

Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,

14

وَمَنْ فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا ثُمَّ يُنْجِيهِ

Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.

15

كَلَّا ۖ إِنَّهَا لَظَىٰ

La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,

16

نَزَّاعَةً لِلشَّوَىٰ

Unao babua ngozi ya kichwa!

17

تَدْعُو مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىٰ

Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.

18

وَجَمَعَ فَأَوْعَىٰ

Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.

19

۞ إِنَّ الْإِنْسَانَ خُلِقَ هَلُوعًا

Hakika mtu ameumbwa na papara.

20

إِذَا مَسَّهُ الشَّرُّ جَزُوعًا

Inapo mgusa shari hupapatika.

21

وَإِذَا مَسَّهُ الْخَيْرُ مَنُوعًا

Na inapo mgusa kheri huizuilia.

22

إِلَّا الْمُصَلِّينَ

Isipo kuwa wanao sali,

23

الَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ دَائِمُونَ

Ambao wanadumisha Sala zao,

24

وَالَّذِينَ فِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ مَعْلُومٌ

Na ambao katika mali yao iko haki maalumu

25

لِلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ

Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;

26

وَالَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ

Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,

27

وَالَّذِينَ هُمْ مِنْ عَذَابِ رَبِّهِمْ مُشْفِقُونَ

Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.

28

إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍ

Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.

29

وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ

Na ambao wanahifadhi tupu zao.

30

إِلَّا عَلَىٰ أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ

Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -

31

فَمَنِ ابْتَغَىٰ وَرَاءَ ذَٰلِكَ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الْعَادُونَ

Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.

32

وَالَّذِينَ هُمْ لِأَمَانَاتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَاعُونَ

Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,

33

وَالَّذِينَ هُمْ بِشَهَادَاتِهِمْ قَائِمُونَ

Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,

34

وَالَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ

Na ambao wanazihifadhi Sala zao.

35

أُولَٰئِكَ فِي جَنَّاتٍ مُكْرَمُونَ

Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.

36

فَمَالِ الَّذِينَ كَفَرُوا قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ

Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?

37

عَنِ الْيَمِينِ وَعَنِ الشِّمَالِ عِزِينَ

Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!

38

أَيَطْمَعُ كُلُّ امْرِئٍ مِنْهُمْ أَنْ يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍ

Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?

39

كَلَّا ۖ إِنَّا خَلَقْنَاهُمْ مِمَّا يَعْلَمُونَ

La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.

40

فَلَا أُقْسِمُ بِرَبِّ الْمَشَارِقِ وَالْمَغَارِبِ إِنَّا لَقَادِرُونَ

Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza

41

عَلَىٰ أَنْ نُبَدِّلَ خَيْرًا مِنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ

Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.

42

فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا وَيَلْعَبُوا حَتَّىٰ يُلَاقُوا يَوْمَهُمُ الَّذِي يُوعَدُونَ

Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,

43

يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ الْأَجْدَاثِ سِرَاعًا كَأَنَّهُمْ إِلَىٰ نُصُبٍ يُوفِضُونَ

Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,

44

خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۚ ذَٰلِكَ الْيَوْمُ الَّذِي كَانُوا يُوعَدُونَ

Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.

Islamic Vault

Quran Explorer

Sumber online lengkap untuk membaca dan mempelajari Al-Quran dengan berbagai terjemahan, transliterasi, dan tilawah dari qari terkenal.

Kitab ini tidak ada keraguan padanya; petunjuk bagi mereka yang bertakwa.

Al-Quran 2:2

Fitur

  • Tilawah Audio
  • Berbagai Terjemahan
  • Transliterasi
  • 114 Surah
  • 6.236 Ayat

© 2026 Islamic Vault. Hak cipta dilindungi.

Dibuat dengan penghormatan dan kehati-hatian untuk Kitabullah

Dikembangkan oleh Medita Development

Penyangkalan: Meskipun kami berusaha untuk akurat, mohon verifikasi informasi agama penting dengan ulama Islam dan sumber terpercaya. Platform ini untuk tujuan pendidikan.