Islamic Vault

Coran

88

Al-Ghaashiya

سورة الغاشية

The Overwhelming26 versets Mecquoise

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ

Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?

2

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ خَاشِعَةٌ

Siku hiyo nyuso zitainama,

3

عَامِلَةٌ نَاصِبَةٌ

Zikifanya kazi, nazo taabani.

4

تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةً

Ziingie katika Moto unao waka -

5

تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ آنِيَةٍ

Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.

6

لَيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِنْ ضَرِيعٍ

Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.

7

لَا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِي مِنْ جُوعٍ

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

8

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَاعِمَةٌ

Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.

9

لِسَعْيِهَا رَاضِيَةٌ

Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,

10

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ

Katika Bustani ya juu.

11

لَا تَسْمَعُ فِيهَا لَاغِيَةً

Hawatasikia humo upuuzi.

12

فِيهَا عَيْنٌ جَارِيَةٌ

Humo imo chemchem inayo miminika.

13

فِيهَا سُرُرٌ مَرْفُوعَةٌ

Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,

14

وَأَكْوَابٌ مَوْضُوعَةٌ

Na bilauri zilizo pangwa,

15

وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌ

Na matakia safu safu,

16

وَزَرَابِيُّ مَبْثُوثَةٌ

Na mazulia yaliyo tandikwa.

17

أَفَلَا يَنْظُرُونَ إِلَى الْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ

Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?

18

وَإِلَى السَّمَاءِ كَيْفَ رُفِعَتْ

Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?

19

وَإِلَى الْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ

Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?

20

وَإِلَى الْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ

Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?

21

فَذَكِّرْ إِنَّمَا أَنْتَ مُذَكِّرٌ

Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.

22

لَسْتَ عَلَيْهِمْ بِمُصَيْطِرٍ

Wewe si mwenye kuwatawalia.

23

إِلَّا مَنْ تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ

Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,

24

فَيُعَذِّبُهُ اللَّهُ الْعَذَابَ الْأَكْبَرَ

Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!

25

إِنَّ إِلَيْنَا إِيَابَهُمْ

Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.

26

ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُمْ

Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!

Islamic Vault

Quran Explorer

Une ressource en ligne complète pour lire et étudier le Saint Coran avec plusieurs traductions, translittérations et récitations audio de récitants renommés.

C'est le Livre au sujet duquel il n'y a aucun doute, une guidance pour les pieux.

Coran 2:2

Fonctionnalités

  • Récitations Audio
  • Traductions Multiples
  • Translittérations
  • 114 Sourates
  • 6 236 Versets

© 2026 Islamic Vault. Tous droits réservés.

Construit avec révérence et soin pour le Livre d'Allah

Développé par Medita Development

Avertissement : Bien que nous nous efforcions d'être précis, veuillez vérifier les informations religieuses importantes auprès de savants islamiques authentiques et de sources fiables. Cette plateforme est à des fins éducatives.

Surah Al-Ghaashiya - Ali Muhsin Al-Barwani Swahili Translation | Islamic Vault | Islamic Vault