Islamic Vault

Coran

83

Al-Mutaffifin

سورة المطففين

Defrauding36 versets Mecquoise

Translated by Ali Muhsin Al-Barwani

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

1

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ وَيْلٌ لِلْمُطَفِّفِينَ

Ole wao hao wapunjao!

2

الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُوا عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَ

Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.

3

وَإِذَا كَالُوهُمْ أَوْ وَزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ

Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.

4

أَلَا يَظُنُّ أُولَٰئِكَ أَنَّهُمْ مَبْعُوثُونَ

Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa

5

لِيَوْمٍ عَظِيمٍ

Katika Siku iliyo kuu,

6

يَوْمَ يَقُومُ النَّاسُ لِرَبِّ الْعَالَمِينَ

Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?

7

كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٍ

Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.

8

وَمَا أَدْرَاكَ مَا سِجِّينٌ

Unajua nini Sijjin?

9

كِتَابٌ مَرْقُومٌ

Kitabu kilicho andikwa.

10

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِلْمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!

11

الَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ

Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.

12

وَمَا يُكَذِّبُ بِهِ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ

Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.

13

إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ

Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!

14

كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِمْ مَا كَانُوا يَكْسِبُونَ

Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.

15

كَلَّا إِنَّهُمْ عَنْ رَبِّهِمْ يَوْمَئِذٍ لَمَحْجُوبُونَ

Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.

16

ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُو الْجَحِيمِ

Kisha wataingia Motoni!

17

ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا الَّذِي كُنْتُمْ بِهِ تُكَذِّبُونَ

Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.

18

كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْأَبْرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ

Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.

19

وَمَا أَدْرَاكَ مَا عِلِّيُّونَ

Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?

20

كِتَابٌ مَرْقُومٌ

Kitabu kilicho andikwa.

21

يَشْهَدُهُ الْمُقَرَّبُونَ

Wanakishuhudia walio karibishwa.

22

إِنَّ الْأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍ

Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.

23

عَلَى الْأَرَائِكِ يَنْظُرُونَ

Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.

24

تَعْرِفُ فِي وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ النَّعِيمِ

Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,

25

يُسْقَوْنَ مِنْ رَحِيقٍ مَخْتُومٍ

Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,

26

خِتَامُهُ مِسْكٌ ۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ الْمُتَنَافِسُونَ

Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.

27

وَمِزَاجُهُ مِنْ تَسْنِيمٍ

Na mchanganyiko wake ni Tasniim,

28

عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا الْمُقَرَّبُونَ

Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.

29

إِنَّ الَّذِينَ أَجْرَمُوا كَانُوا مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا يَضْحَكُونَ

Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.

30

وَإِذَا مَرُّوا بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ

Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.

31

وَإِذَا انْقَلَبُوا إِلَىٰ أَهْلِهِمُ انْقَلَبُوا فَكِهِينَ

Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.

32

وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوا إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَضَالُّونَ

Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.

33

وَمَا أُرْسِلُوا عَلَيْهِمْ حَافِظِينَ

Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.

34

فَالْيَوْمَ الَّذِينَ آمَنُوا مِنَ الْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ

Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,

35

عَلَى الْأَرَائِكِ يَنْظُرُونَ

Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.

36

هَلْ ثُوِّبَ الْكُفَّارُ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ

Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?

Islamic Vault

Quran Explorer

Une ressource en ligne complète pour lire et étudier le Saint Coran avec plusieurs traductions, translittérations et récitations audio de récitants renommés.

C'est le Livre au sujet duquel il n'y a aucun doute, une guidance pour les pieux.

Coran 2:2

Fonctionnalités

  • Récitations Audio
  • Traductions Multiples
  • Translittérations
  • 114 Sourates
  • 6 236 Versets

© 2026 Islamic Vault. Tous droits réservés.

Construit avec révérence et soin pour le Livre d'Allah

Développé par Medita Development

Avertissement : Bien que nous nous efforcions d'être précis, veuillez vérifier les informations religieuses importantes auprès de savants islamiques authentiques et de sources fiables. Cette plateforme est à des fins éducatives.